Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Juni, 2019

Vyakula vinavyoongeza uwezo wa kuona

Picha
Je unakula chakula bora ambacho ni bora pia kwa ajili ya macho yako? Kula vizuri kuna manufaa mengi kwa ajili ya miili yetu; macho nayo yakiwemo. Kuna virutubisho mbalimbali vinavyohitajika kwenye macho kuliko tu vile vinavyofahamika na wengi vilivyoko kwenye karoti. Jifunze ni vyakula gani vitayapa macho yako na kuyawezesha kupata virutubisho ambavyo vitayalinda dhidi ya kupungua kwa uwezo wa kuona. Samaki Samaki ni chakula bora kwa afya ya macho hasa wale wa maji baridi, kwani wamejaa asidi ya mafuta ya omega-3 ambayo ni muhimu kwa ajili ya kuzuia macho angavu (kunyauka kwa macho), kudhoofu kwa misuli ya macho na hata mtoto wa jicho. Kama umeshindwa kula vyakula hivi vya baharini unaweza kula matunda kama vile matunda damu ili kupata asidi ya mafuta ya omega-3. Mboga za majani Watu wengi hufikiri kuwa kula mboga za majani ni umaskini; lakini ukweli ni kuwa mboga za majani zina manufaa makubwa kwenye miili yetu. Mboga za majani zina kemikali ya luteini na zeaxanthini ambazo n...

Tatizo la Unyafuzi

Picha
Unyafuzi ,  chirwa  au  kwashakoo  ni aina kali ya  utapiamlo  inayosababishwa na ukosefu wa  protini  ya kutosha katika  chakula . Dalili  ya unyafuzi ni upungufu wa  uzito , kuchoka sana, na uvimbe wa  tumbo . Nywele kunyonyoka Njia pekee ya kupambana na tatizo hili ni kula vyakula vilivyo na protein ya kutosha Kama Nyama  za aina mbalimbali ( ng'ombe ,  kuku ,  mbuzi ,  samaki ,  maini  na kadhalika),   maharagwe ,  maziwa , na  mayai .

Vyakula vya kuongeza nguvu za kiume

Picha
Nguvu za kiume ni neno linalotumika mara nyingi kumaanisha ‘Uwezo wa mwanaume kufanya tendo la ndoa’. Na inapokuwa tofauti na hivi, tunaita ni ‘kupungua au kukosa nguvu za kiume’. Kupungukiwa kwa nguvu za kiume hutofautiana toka mtu mmoja hadi mwingine. Inaweza kuwa ni hali ya kutokuwa na uwezo wa kusimamisha uume, au hali ya kutokuwa na uwezo wa kufika kileleni kwa muda mzuri wa kutosha. Pamoja na hayo yote, elimu mhimu ambayo mwanaume anatakiwa kuwa nayo, ni kuwa nguvu za kiume hazipatikani kwa kutumia madawa ya kemikali au mahala pengine; bali zinatokana na vyakula tunavyokula kila siku. 1. Kitunguu swaumu Chukuwa punje 8 mpaka 10 za kitunguu swaumu, menya na uzikate vipande vidogo vidogo kisha meza na maji vikombe 2 kutwa mara 2 kwa mwezi mmoja. Pia hakikisha kila chakula unachopika basi kitunguu swaumu lazima kiwemo kama moja ya viungo na ukiweke mwishoni mwishoni kwamba kisiive sana katika moto wakati unapika hicho chakula. 2. Tikiti maji Kula tikiti maji k...

Lishe kwa mgonjwa wa Kisukari

Picha
Ugonjwa wa kisukari ni tatizo ambalo siku hizi husababishwa na mfumo wa maisha tunayoishi hasa vijana, tafiti zilizowahi kufanywa zinaonesha kuwa vijana wapo kwenye hatari kubwa ya kupata kisukari kwa sababu ya mfumo usio sahihi wa maisha wanayoishi vijana. Kutokufanya mazoezi, kukosa muda wa kupumzika na kutokula mlo sahihi,unywaji wa pombe na uvutaji sigara wa kupitiliza, hizi ni sababu chache zinazochangia vijana kuishi katika mfumo wa maisha hatarishi wa kupata maradhi ya kisukari. Leo tunaangalia suala zima la chakula kwa watu mwenye maradhi ya kisukari,madaktari wapo wengi sana kwenye hospitali zetu pamoja na majumbani mwetu lakini wewe mwenye ugonjwa wa  kisukari ndiyo daktari namba moja katika kutibu afya yako. Kitu muhimu kwa mgonjwa wa kisukari ni  kufahamu ya kwamba  ana uwanja mpana  sana wa vyakula anavyoruhusiwa kula tofauti na  na mazoea yaliyojengeka miongoni mwetu kuwa mtu anayeuugua maradhi haya basi ana  vyakula vyake vya kipekee...